English Home Romanian Home
Electronic Bible Online Pages Multi Language Phone Application One Language d/">Download Ipod / MP4 Player Package Electronic Online Mobile Pages
Electronic Books Online Pages Build Ebook Phone Application Download Ebook Phone Application Download Desktop Application Download Ipod / MP4 Player Package Electronic Online Mobile Pages
Create Bible Application Create E-Books Application
Credits News
About our project   |    Mobile Pages   |   
Electronic Bibles / Swahili / Swahili Union Bible / Web / Kumbukumbu la Torati

Swahili

Printable ModePrintable Mode

Kumbukumbu la Torati, Chapter 23

23:1 Aliyejeruhika konde, au aliyekatika tupu yake, asiingie mtu huyo katika mkutano wa Bwana.

23:2 Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa Bwana.

23:3 Mwamoni wala Mmoabi wasiingie katika mkutano wa Bwana; wala hata kizazi cha kumi mtu wao asiingie katika mkutano wa Bwana milele;

23:4 kwa sababu hapo mlipotoka Misri hawakuwalaki na chakula wala maji njiani; na kwa kuwa walimwajiri juu yako Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyo Mesopotamia, aje akuapize.

23:5 Lakini Bwana, Mungu wako, hakukubali kumsikiza huyo Balaamu; Bwana, Mungu wako, aliyageuza yale maapizo kuwa ni baraka, kwa vile alivyokupenda Bwana, Mungu wako.

23:6 Usitafute amani yao wala heri yao siku zako zote, milele.

23:7 Usimchukie Mwedomi; kwa kuwa ni ndugu yako; usimchukie Mmisri, kwa kuwa ulikuwa mgeni katika nchi yake.

23:8 Wana wao watakaozaliwa kizazi cha tatu na waingie katika mkutano wa Bwana.

23:9 Utakapotoka kwenda juu ya adui zako nawe u katika marago, jilinde na kila neno baya.

23:10 Akiwa kwenu mtu awaye yote asiyekuwa ni tohara kwa ajili ya yaliyomtukia usiku, na atoke nje ya kituo, wala asiingie ndani ya kituo;

23:11 lakini na iwe ikaribiapo jioni, yeye ataoga maji; na jua likiisha kuchwa ataingia ndani ya kituo.

23:12 Tena uwe na mahali nje ya kituo, kwa kutokea nje;

23:13 nawe uwe na jembe dogo katika silaha zako; napo uotamapo nje uchimbe kwa lile jembe, na kugeuka na kukifunika kikutokacho;

23:14 kwa kuwa Bwana. Mungu wako, yuatembea katika kituo akuokoe, na kukutolea adui zako mbele yako; kwa hiyo na kiwe kitakatifu kituo chako; asije akaona kitu kwako kisichokuwa safi, akageuka na kukuacha.

23:15 Usimrudishe kwa bwana wake mtumwa aliyejiponya kutoka kwa bwana wake kuja kwako;

23:16 na akae nawe, katikati yako, ndani ya malango yako mojawapo, mahali atakapochagua palipo pema machoni pake; usimwonee.

23:17 Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume.

23:18 Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili.

23:19 Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;

23:20 mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki.

23:21 Utakapoweka nadhiri kwa Bwana, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako.

23:22 Lakini ukijizuia usiweke nadhiri, haitakuwa dhambi kwako.

23:23 Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako.

23:24 Uingiapo katika shamba la mizabibu la jirani yako, utaweza kula zabibu za kukushibisha, kama upendavyo; ila usitie katika chombo chako.

23:25 Uingiapo katika mmea wa jirani yako waweza kuyapurura masuke kwa mkono wako; ila usisongeze mundu katika mmea wa jirani yako.

Printable Mode

Seek to any passage:


Book:
Chapter:
Verse:


Search the text:


Search in:
Terms:
Case insensitive:

Multilingual Online Bibles

It is possible now to have the Holy Scriptures on your browser and to read it by using parallel display that will allow you to make comparisons between different translations or versions for a specific language. This occasion is unique, and you have only to add new parallel versions from the left side "Add parallel language" selector.


Select another version:


Add parallel versions:


Delete parallel versions:


Text source: This text is in the public domain, downloaded from http://www.unboundbible.org, compiled by biblephone2008@gmail.com.





free counters

Locations of visitors to this page






If you have any questions, remarks, suggestions, please contact me here. May God bless you in studying the Holy Scriptures.



Sitemap: Please select the BiblePhone modules in your language: